Monday, 7 November 2016

MWANAUME UWE NA MSIMAMO KAMA HUU

*MAMA MKWE* 👂🏾


_Ilikuwa wakati wa mchana ambapo mume alirejea nyumbani akiwa na habari mbaya._

*MUME:* _Mpenzi, nimepigiwa simu: Mama hajisikii vizuri. Tunaweza kwenda kumnunulia baadhi ya mahitaji kwa ajili ya kumtembelea?_

```Tafadhali andika orodha ya mahitaji kisha tuondoke.```



*MKE:* _Orodha ya vitu hivyo sio muhimu, tutanunua tu kabichi 2 na lita 2 za mafuta ya kupikia._

*MUME:* _Vitatosha kweli?_

*MKE:* _Ndiyo mpenzi, hakuna haja ya kupoteza pesa, vitatosha._

```Walielekea mjini na kununua kabichi 2 na lita 2 za mafuta ya kupikia. Wakati wakinunua mume alimuuliza mkewe tena kama vitu hivyo vingetosha.```


_Mke alisisitiza zaidi kuwa hawatakiwi kutumia pesa nyingi kwenye ziara ya kushtukiza._

```Walianza safari kuelekea kijijini, na walipofika kwenye eneo la njia panda yenye barabara zinazoelekea vijiji mbalimbali, mume alikata kona kuelekea kwao na mke.```

*MKE:* _(Kwa mshituko) tunaelekea wapi mpenzi? Nilidhani tunaenda kumtembelea mama yako._

*MUME:* _Ndiyo, ndiko tunakuelekea. Ni mama yako (mama yetu) ndiye anayeumwa._

*MKE:* _(kwa mshituko na kilio), lakini mahitaji haya hayatoshi. Turudi tuongeze vitu vingine._

*MUME:* _Hapana! Nilikuuliza tena na tena kama mahitaji hayo yanatosha, ukaniambia “NDIYO”. Hakuna kurudi….._

```FUNZO:```

```Wafanyie wenzako kile unachotaka ufanyiwe!!```

*Yes, hatupendagi ubaguzi sisi.*
🙈🙈🙈‼

The Author

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Morbi eu sem ultrices, porttitor mi eu, euismod ante. Maecenas vitae velit dignissim velit rutrum gravida sit amet eget risus. Donec sit amet mollis nisi, nec commodo est.

No comments:

Post a Comment

[Latest News][6]

Featured

Featured

Header Ad Widget

Pages

Label Icons CSS

Videos